
Hayo ndiyo mapenzi jamani!
Tumekua tukisikia na kuona hata kwa ndugu jamaa na marafiki namna wapenzi
wanavyo lalamika kwa watu walio karibu nao.
Lakini pia katika kufurukuta
kumtafuta mpenzi wa kuwa naye maishani, mwanaume anaweza kujikuta unaangukia
kwa msichana ambaye tayari ameshatoka kuumizwa pasipo rasmi ya kuachana na
ndipo pia msichana kujikuta akiingia kirahisi kwa kufikiri kutuliza maumivu ya
wakati huo pasipo kujipa muda kwa kisingizio cha kua na stress.
Moyo wako unakuambia yeye ndiye
mtu sahihi katika maisha yako lakini tayari ana mtu wake, unafanyaje?


Utapambana kuhakikisha unapata
kile ambacho moyo wako umekipenda au utakubaliana na ukweli kwamba huwezi kuwa
naye kwa kuwa ana mahusiano na msichana mwingine walioukua wamehskua mbali
lakini pande moja inavuta kurudi walikokua mwanzo hapo unakuja kugundua kua
kumbe ulipoingia nay eye ana mtu wake. Inapofikia hatua hiyo unaweza kujikuta
upo njia panda hasa pale ambapo huyo mwenye mtu wake naye anaonesha kuwa na
chembechembe za mapenzi kwako pamoja na kukupa fursa ya kua wewe ndio chaguo
lake.
Chunguza
Unapojikuta umeingia katika
mahusiano mapya usijikite moja kwa moja kwa siku moja au wiki kujiona umefika mahali
ulipotegemea cha kwanza tumia muda wako mwingi kuchunguza juu ya uhusiano wake
wa awali kama ulishakoma au bado kuna chembe chembe za mawasiliano na ni kwa
muda gani.
Uhusiano wao umesimama na
wanaonekana ni watu wenye ‘future’? Nasema hivyo kwa sababu, yawezekana
uhusiano wa huyo uliyetokea kumpenda ni wa kuzuga tu na huenda wewe ndiye
mwenye ‘future’ naye nay eye asilitambue hilo. Ndiyo maana nikasema chunguza
uhusiano wake kwanza.
Usitafute uadui
Baada ya kuchunguza, ukibaini
kwamba uhusiano wao hauko ‘siriasi’, vuta subira, lolote linaweza kutokea na
likaufurahisha moyo wako. Lakini kama utaona ni watu walio siriasi na wanaendelea
na mawasiliano ya maara kwa mara kwa kupigiana simu kuchati au hata kuonana,
usitafute uadui bure, kaa pembeni.


Una nafasi kwake?
Sawa umetokea kumpenda msichana/mvulana
aliye mpya kwako, umeshawahi kujiuliza kama una nafasi ndani ya moyo wake?
Anaonesha dalili fulani za kukupenda kama unavyompenda na ni mtu anayeonesha
kukumisi anapokuwa mbali na wewe? Utakapobaini una nafasi kwake, uamuzi wa
kumpotezea hautakuwa na nafasi.


Ni rahisi kubadili uamuzi wake?
Unadhani huyo uliyetokea kumpenda
anaweza kubadili maamuzi ya kuacha mambo unayoweza kuyaona hayafai mbele ya
uhusiano wenu mambo yanayoweza kuhatarisha uhusiano wenu kuyumba, kama kweli hana
‘future’? Utagundua hilo kwa kuongea naye na kumsikia kama anaweza kufanya
maamuzi hayo ili awe na wewe.


Pingana na moyo wako
Ifike wakati upingane na moyo
wako. Unajua moyo wako kukuambia kuwa unataka kuwa na uhusiano na msichana au
mvulana ambaye tayari ana ameachana au anampenzi wake wakati mwingine utakuwa
unakupotosha.
Kwa hiyo ukiona vipi, pingana
nao. Acha kumng’ang’ania msichana/mwanaume mwenye mpenzi wake licha ya ukweli
kwamba, huenda wewe ndiye mwenye nafasi ya kuwa mume/mke wake na siyo huyo
aliye naye.


Urafiki ni sawa?
Umempenda sana na hauko tayari
kumkosa katika maisha yako lakini imetokea kwamba tayari yuko na mtu na
umebaini huna nafasi kwake kabisa? Usiumie, omba angalau urafiki. Siyo urafiki
wa kivile sana ila angalau pale unapotaka kusikia sauti yake kwa kumsalimia tu,
upate nafasi hiyo.


Usiumie, yupo mwingine
Haina haja ya kujitafutia vidonda
vya tumbo bure wala kujipa stress kwenye maisha yako kwa kuwa tu umebaini
uliyetokea kumpenda tayari ana mtu. Chukulia ni hali ya kawaida, wakati
mwingine moyo husukuma sana na kuumia kwa kujiona umenyanyaswa lakini si jambo
la kuweka sana katika moyo na akili yako cha msingi ni kufocus na kutazama
mbele. Wanaume na wasichana wazuri ambao wanaishi singo wapo kibao huko mtaani,
ni suala la wewe kutulia tu. Amini yupo mwingine ambaye atayafanya maisha yako
yawe ya furaha.


Naomba nihitimishe kwa kusema
kwamba, unapotokea kumpenda mtu fulani, pambana kuhakikisha unampata kwa sababu
ukimkosa maisha yako yanaweza kuwa gizani. Ila pale utakapoona uwezekano wa
kuwa naye haupo, usilazimishe ndugu yangu. Kumbuka haya ni maisha tu!
Love Clinic inakukaribisha sana
kutembelea blog hii kila mara ili uweze kuelimika Zaidi kila siku na kujifunza
changamoto mbali mbali ili nawe uweze kuzishinda.
Tunakushauri kama unajambo
lolote, swali, changamoto, maoni na ushauri, ama tukio lolote ilimradi liwe la
kweli tunakukaribisha katika safu ya ukurasa wetu.
Wasiliana nasi kwa:
Email: mossesshio@gmail.com
Whatsapp: +255745222780
0 comments :
Post a Comment