KWANINI UVAE NGUO FUPI MWENYEWE HALAFU UKOSE AMANI



Hivi huu ni ulimbukeni wa mavazi au ni kuiga tabia zisizo na kichwa wala miguu???
Tabia za wadada wengi hasa wa mijini

Baadhi ya Wadada wa Darisalamu shida kweli, sasa nguo fupi umevaa mwenyewe ya nini kuhangaika kushusha shusha chini unavotembea. Wenzenu hizo wanavaaga wakiwa na magari yao wakielekea maeneo ya hadhi zao, sasa wewe nawe na kinguo chako kifupi unapanda basi la mwendokasi kuelekea Karume kununua mitumba huku ukikazana kuvuta chini kisketi chako kifupi, kwani ulivalishwa?

Kama umeamua kuwafaidisha watu waache wafaidi, kwanini msivae nguo zenye heshima na kuwastiri miili yen utu usiangaike kuvuta chini. Hizo akili sijui hua mnafungiaga kwenye kabati mkiondoka makwenu? mnavuruga akili na swaumu za watu mjue. vaa nguo ambayo utakua comfortable nayo!!!

Wanawake wengi mpaka mnakua mnajidhalilisha wenyewe halafu mkiambiwa mnaona kama mmekosewa hebu jiheshimuni jamani kwa wakati huu sio wa kati wa kuoneshana vichupi au mapaja yenu. Muwe na siku njema


Wewe mwanadasa unaejitambua hebu ungana na Love Clinic kukemea hali hii ya wadada wenzio sisi wanume tumechokaaa!!!!!!
Share on Google Plus

About Mlaki

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment